• HABARI MPYA

    Friday, August 01, 2014

    BEKI LA ARSENAL LATUA WEST HAM

    KLABU ya West Ham imemsajili kwa mkopo wa muda mrefu beki wa kulia wa Arsenal, Carl Jenkinson. 
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 amekubaliwa kuondoka Emirates kufuatia kuwasili kwa Calum Chambers kutoka Southampton na Mathieu Debuchy kutoka Newcastle.
    Hull City imepiga hatua zaidi kutaka kumsajili moja kwa moja mchezaji huyo wa kimataifa wa England lakini inasuasua kufika bei ya Pauni Milioni 3.

    Ofisi mpya: Carl Jenkinson ametambulishwa kuwa mchezaji mpya wa West Ham jana
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI LA ARSENAL LATUA WEST HAM Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top