Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MSHAMBULIAJI wa Ruvu Shooting, Elias Maguri amesaini Mkataba wa miaka miwil kujiunga na Simba SC.
Maguri aliyechezea Prisons ya Mbeya awali, amesema; “Kutua Simba SC ni ndoto yangu ya muda mrefu sana tangu nipo mdogo nilikuwa ninaota kuchezea timu kubwa,”.
Aidha Maguri akizungumza na BIN ZUBEIRY baada ya kumalizana na Simba SC, amesema kwamba anafahamu changamoto inayomkabili baada ya kusaini timu hito kubwa na amejiandaa vyema kukabiliana nayo.
“Simba SC ni timu kubwa na ina wachezaji wakubwa, wa hapa hapa nyumbani na wa kigeni pia, yote ninayajua na kwa kuwa najiamini ndiyo maana sikusita kusaini,”amesema.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba mshambuliaji huyo ni kijana mdogo ambaye wanaamini atakuwa na wakati mzuri kwenye klabu yao.
“Maguri bado ni kijana mdogo, akiwa Simba SC atakuwa na fursa nzuri ya kuongeza ujuzi na uzoefu wake kisoka,”amesema.
Kipaji hicho kutoka mkoani Mara kilichototokea kwenye mtandao wa mashindano ya vijana ya Copa Coca Cola, msimu uliopita kilikuwemo kwenye timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha Mdenmark, Kim Poulsen.
Januari mwaka huu alikwenda Oman kujaribu kujiunga na Seeb ya Ligi Kuu ya huko, lakini akafeli majaribio.
Aliporejea nchini, aliingia kwenye mtafaruku na klabu yake, Ruvu Shooting kwa kuondoka bila kuaga, kabla ya kumalizana na kuendelea kucheza.
MSHAMBULIAJI wa Ruvu Shooting, Elias Maguri amesaini Mkataba wa miaka miwil kujiunga na Simba SC.
Maguri aliyechezea Prisons ya Mbeya awali, amesema; “Kutua Simba SC ni ndoto yangu ya muda mrefu sana tangu nipo mdogo nilikuwa ninaota kuchezea timu kubwa,”.
Aidha Maguri akizungumza na BIN ZUBEIRY baada ya kumalizana na Simba SC, amesema kwamba anafahamu changamoto inayomkabili baada ya kusaini timu hito kubwa na amejiandaa vyema kukabiliana nayo.
Ametua Msimbazi; Elias Maguri amesaini miaka miwili Simba SC |
“Simba SC ni timu kubwa na ina wachezaji wakubwa, wa hapa hapa nyumbani na wa kigeni pia, yote ninayajua na kwa kuwa najiamini ndiyo maana sikusita kusaini,”amesema.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba mshambuliaji huyo ni kijana mdogo ambaye wanaamini atakuwa na wakati mzuri kwenye klabu yao.
“Maguri bado ni kijana mdogo, akiwa Simba SC atakuwa na fursa nzuri ya kuongeza ujuzi na uzoefu wake kisoka,”amesema.
Maguri kushoto akisaini na Kaburu leo Msimbazi |
Kipaji hicho kutoka mkoani Mara kilichototokea kwenye mtandao wa mashindano ya vijana ya Copa Coca Cola, msimu uliopita kilikuwemo kwenye timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha Mdenmark, Kim Poulsen.
Januari mwaka huu alikwenda Oman kujaribu kujiunga na Seeb ya Ligi Kuu ya huko, lakini akafeli majaribio.
Aliporejea nchini, aliingia kwenye mtafaruku na klabu yake, Ruvu Shooting kwa kuondoka bila kuaga, kabla ya kumalizana na kuendelea kucheza.
0 comments:
Post a Comment