KLABU ya Swansea City imekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 8 wa Federico Fernandez kutoka Napoli.
Beki huyo wa kati alikwenda kufanyiwa vipimo vya afya wiki hii Wales na kusaini Mkataba wa miaka minne, akiweka rekodi ya kuwa mchezaji ghali zaidi wa nafasi za ulinzi kusajiliwa na klabu za Wales.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye aliichezea Argentina katika Kombe la Dunia, ataziba pengo la beki wa kati Chico Flores aliyeondoka, kwa kucheza na Ashley Williams.
0 comments:
Post a Comment