MSHAMBULIAJI Alexis Sanchez leo ameanza mazoezi Arsenal kujiandaa na michuano ya Kombe la Emirates.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 30 The Gunners kutoka Barcelona alijifua na timu yake mpya kwa mara ya kwanza.
Sanchez (kulia) anaweza kupangwa kwenye mechi dhidi ya Benfica kesho katika Kombe la Emirates
Sanchez (kulia) alisajiliwa na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger (kushoto) kwa Pauni Milioni 30 mwezi Julai
Sanchez (kulia) akijifua pembeni rya Mathieu Flamini (kushoto)
Sanchez alikosa ziara ya siku nne ya timu hiyo Marekani wiki iliyopoita, katokana na kupewa mapumziko ya baada ya Kombe la Dunia, lakini aliripoti Jumanne tayari kuanza mazoezi.
Mshambuliaji huyo wa Chile amekuwa akifanya mazoezi maalum ya kumuweka fiti chini ya wasaidizi wa Arsene Wenger na anatarajiwa kuichezea kwa mara ya kwanza klabu hiyo kesho dhidi ya Benfica.
0 comments:
Post a Comment