KOCHA Arsene Wenger amempa jezi namba 23 mshambuliaji mpya alyemsajili kwa Pauni Milioni 16kutoka Manchester United, Danny Welbeck.
Welbeck, ameamua kuondoka Old Trafford baada ya kuona hana nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Mholanzi, Louis van Gaal na alilazimisja uhamisho wa moja kwa moja baada ya awali, United kutaka kumtoa kwa mkopo wa Pauni Milioni 3 Arsenal.
Welbeck anakwenda kuanza maisha mapya The Gunners baada ya kusaini Mkataba wa miaka mitano akiwa na matumaini makubwa ya kung'ara kutokana na mapungufu ya washambuliaji Arsenal.
Namba ya jezi: Welbeck amechukua jezi namba 23, ambayo ilipatiwa umaarufu na mcheza mpira wa kikapu Michael Jordan na baadaye kiungo David Beckham
0 comments:
Post a Comment