KLABU ya Arsenal inapambaa dakika za mwishoni kuelekea kufungwa dirisha la usajili kuhakikisha inakamilisha uhamisho wa mshambuliaji wa Manchester United, Danny Welbeck kwa dau la Pauni Milioni 6.
Hiyo inafuatia The Gunners kumkosa mshambuliaji wa Monaco, Radamel Falcao, ambaye amehamia Manchester United leo.
Hivi sasa inaelezwa Welbeck anafanyiwa vipimo vya afya Arsenal kukamilisha uhamisho huo.
0 comments:
Post a Comment