• HABARI MPYA

    Tuesday, October 21, 2014

    MAYWEATHER ANA BAHATI SANA YA KUPIGA 'MAHELA' HUYU JAMAA, ONA SASA KAMA HIZI ZA NFL ALIZOLAMBA KIULAINI BILA HASHO

    WAHENGA walisema, mwenye nacho huongezewa- usemi huo unadhihirika kwa mara nyingine kupitia bondia Floyd Mayweather Jnr ambaye kishinda kitita ch fedha baada ya kubeti kwenye mchezo wa NFL.
    Bingwa huyo wa madaraja matano tofauti ya uzito wa ndondi duniani, ambaye tayari ni mwanamichezo tajiri ulimwenguni, sasa ameshinda kiasi cha dola za Kimarekani Milioni 4 katika beti zake za wiki za karibuni.
    Mafanikio mapya ya Mayweather yanakuja baada ya kuweka dola 800,000 katika mchezo ambao Arizona Cardinals imeifunga Oakland Raiders.
    Mayweather hive karibuni aliposti picha kwenye mitandao ya kijamii akiwa ametandaza fedha
    Floyd Mayweather bets on Denver Bronco's new York Jets game winning $1.4m
    Risiti za Mayweather katika kubeti ambazo zimemuingizia mamilioni ya dola

    Cardinals ilishinda 24-13, maana yake Mayweather amevunja zaidi ya cola Milioni 1.5 na kama kawaida yake, 'Mtu Fedha' huyo akaposti kwenye akaunti yake ya Twitter kusherehekea mafanikio hayo pamoja na watu Miloni 5.34 wanaomfolo.
    Mayweather aliingiza cola Milioni 105 katika pambano lake na Saul Alvarez na la ushindi wake wa kwanza dhidi ya Marcos Maidana na sasa anajiandaa kwa pambano lingine Mei, mwakani.
    Bondia huyo mwenye umri wa miaka 37 amebakiza mapambano mawili katika Mkataba wake wa mapambano sita na Showtime na amesema baada ya halo atastaafua. Moja ya mapambano yake mawili linatarajiwa kuwa dhidi ya Muingereza Amir Khan mjini Las Vegas Mei mwakani.
    Arizona Cardinals celebrate during their victory over the Oakland Raiders as Mayweather cashed in
    Arizona Cardinals wakishangilia ushidi wao dhidi ya Oakland Raiders ambao umempoa fedha Mayweather 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAYWEATHER ANA BAHATI SANA YA KUPIGA 'MAHELA' HUYU JAMAA, ONA SASA KAMA HIZI ZA NFL ALIZOLAMBA KIULAINI BILA HASHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top