• HABARI MPYA

    Thursday, November 27, 2014

    ARSENAL YATINGA 16 BORA LIGI YA MABINGWA BAADA YA KUICHAPA 2-0 DORTMUND

    WASHIKA Bunduki, Arsenal wamefuzu kuingia hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Borussia Dortmund Uwanja wa Emirates katika mchezo wa Kundi.
    Yaya Sanogo aliifngia Arsenal bao lake la kwanza kwenye mechi ya mashindano dakika ya pili, ingawa kinda huyo Mfaransa alionekana kama alikuwa ameotea.
    Alexis Sanchez akaifungia timu ya Arsene Wenger bao la pili dakika ya 57 na kuihakikishia kuingia hatua hiyo ya mtoano. 
    Kikosi cha Arsenal kilikuwa; Martinez, Chambers, Mertesacker, Monreal, Gibbs, Arteta/Flamini dk66, Oxlade-Chamberlain/Campbell dk89, Ramsey, Cazorla, Sanchez, Sanogo/Podolski dk78.
    Borussia Dortmund; Weidenfeller, Piszczek, Subotic, Ginter, Schmelzer, Gundogan, Bender, Grosskreutz, Immobile/Kagawa dk60, Mkhitaryan na Aubameyang/Ramos dk60. 
    Alexis Sanchez runs towards the Arsenal fans in celebration of his second half strike against Borussia Dortmund
    Alexis Sanchez akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la pili dhidi ya Borussia Dortmund
    Sanogo shoots past Dortmund keeper Weidenfeller (right) to score the opening goal of the game
    Sanogo akifumua shuti kumtungua kipa wa Dortmund, Weidenfeller (kulia) kuifungia Arsenal bao la kwanza

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2850813/Arsenal-2-0-Borussia-Dortmund-Yaya-Sanogo-Alexis-Sanchez-strike-secure-16-spot-Arsene-Wenger-s-side.html#ixzz3KDZpStfW 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YATINGA 16 BORA LIGI YA MABINGWA BAADA YA KUICHAPA 2-0 DORTMUND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top