• HABARI MPYA

    Thursday, December 18, 2014

    LIVERPOOL YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, ITAVAANA NA CHELSEA

    LIVERPOOL imetinga Nusu Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu Capital One Cup baada ya kuichapa mabao 3-1 Bournemouth usiku wa jana.
    Kwa ushindi huo, Liverpool itakutana na Chelsea katika Nusu fainali ya michuano hiyo. Raheem Sterling alifunga bao la kwanza zuri dakika ya 20, kabla ya Lazar Markovic kufunga la pili dakika saba baadare. Sterling akafunga la tatu dakika ya 51 kabla ya kiungo wa zamani wa Everton, Dan Gosling kuwafungia wapinzani bao la kufutia machozi dakika ya 57.
    Kikosi cha Bournemouth kilikuwa: Boruc, Francis, Elphick, Cargill, Smith, Ritchie, Gosling, O'Kane/Pitman dk81, Stanislas/Fraser dk54, Wilson, Kermorgant/Arter dk53.
    Liverpool: Jones, Toure, Skrtel, Lovren/Sakho dk45, Henderson, Gerrard/Borini dk90, Lucas, Markovic, Coutinho/Can dk74, Lallana na Sterling.
    England forward Sterling runs off to celebrate giving Liverpool a 3-0 lead against their Championship opponents
    England forward Sterling runs off to celebrate giving Liverpool a 3-0 lead against their Championship opponents

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2878102/Bournemouth-1-3-Liverpool-Raheem-Sterling-scores-twice-Brendan-Rodgers-reach-Capital-One-Cup-semi-finals.html#ixzz3MDjX9SOG 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, ITAVAANA NA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top