• HABARI MPYA

    Wednesday, December 17, 2014

    REAL MADRID YAPIGA MTU 4-0 NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA DUNIA

    KLABU ya Real Madrid usiku wa jana imeichapa mabao 4-0 Cruz Azul na kutinga Fainali ya Klabu Bingwa ya Dunia.
    Beki Sergio Ramos aliifungia Real Madrid bao la kuongoza dakika ya 15 kabla ya Karim Benzema kufunga la pili dakika ya 36.
    Kipa wa Real, Iker Casillas aliokoa mkwaju wa penalti wa Gerardo Torrado dakika chache kabla ya mapumziko baada ya rafu ya Ramos na Gareth Bale akafunga bao la tatu dakika ya 50, kabla ya kiungo Isco kufunga la nne dakika ya 72.
    Kikosi cha Real Madrid kilikuwa; Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos/Varane dk65, Marcelo, Kroos/Khedira dk73, Isco/Jese dk76, Illarramendi, Ronaldo, Bale na Benzema 
    Cruz Azul: Corona, Pinto, Rodriguez, Dominguez, Torrado, Pavone/Barrera dk65, Gimenez/Fabian dk65, Rojas/Valadez dk76, Flores, Bernardello na Formica.
    Bale (third from right) is congratulated by his team-mates after heading Real Madrid into a 3-0 lead after 50 minutes
    Bale (third from right) is congratulated by his team-mates after heading Real Madrid into a 3-0 lead after 50 minutes

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2876495/Real-Madrid-4-0-Cruz-Azul-Gareth-Bale-Karim-Benzema-Sergio-Ramos-Isco-target.html#ixzz3M8GwKFLt 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID YAPIGA MTU 4-0 NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top