• HABARI MPYA

    Wednesday, April 01, 2015

    KAGERA SUGAR YAIPIGA 2-1 MTIBWA SUGAR KAMBARAGE

    Na Philipo Chimi, SHINYANGA
    KAGERA Sugar imewafunga ndugu zao Mtibwa Sugar mabao 2-1 jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
    Kagera walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Andrew Chikope wa Mtibwa aliyejifunga dakika ya 37, kabla ya Ame Ally kuisawazishia Mtibwa dakika ya 47.
    Rashid Mandawa aliifungia bao la ushindi Kagera dakika ya 74.
    Kagera Sugar wameifunga 2-1 Mtibwa Sugar leo

    Kikosi cha Kagera Sugar kilikuwa; Andrwe Ntalla, Benjamin Asukile, Salum Kanoni, Erick Kyaruzi, Georg Kavilla, Malegesi Mwangwa, Juma Mpola/Erick Muliro, Babu Ally, Radhid Mandawa, Atupele Green/Paul Maona na Adam Kigwande/Victor Hangaya.
    Mtibwa Sugar; Abdallah Mangana, Said Mkopi, Majaliwa Mbanga, Andrew Chikopi, Salim Mbonde, Henry Joseph, Ally Shariff, Muzamil Selemba, Ame Ally, Mohamed Ibrahim, Jamal Mnyate/Vincent Barnabas.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAGERA SUGAR YAIPIGA 2-1 MTIBWA SUGAR KAMBARAGE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top