KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho ameteuliwa kuwa kocha Bora wa msimu wa Ligi Kuu ya England, huku nyota wake Eden Hazard akitwaa tuzo ya Mchezaji Bora.
Kocha huyo Mreno aliyeisaidia The Blues kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitano katika msimu ambao wameweka rekodi ya kuwa kileleni kwa siku 274.
Hii ni mara ya tatu kwa Mourinho kutwaa tuzo ya kocha Mkuu Bora wa msimu - awali katika misimu ya mwaka 2004-2005 na 2005-2006.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho akisherehekea tuzo ya Kocha Bora wa msimu (wengine kutoka kushoto) kocha wa makipa, Christophe Lollichon, kocha wa mazoezi ya nguvu, Carlos Lalinn na Makocha Wasaidizi Silvino Louro, Rui Faria, Steve Holland na Chris Jones PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment